Jeshi la Mali lauwa wapiganaji 30

In Kimataifa

Vikosi vya mali vimewauwa kiasi ya wanamgambo 30 katika operesheni yake iliyoendeshwa jana, hayo yakiwa ni machafuko ya hivi karibuni kabisa katika taifa hilo lililovurugwa na vita. Katika ukurasa wake wa Twitter jeshi la nchi hiyo limesema limefanya mauwaji hayo katika eneo na Burkina Faso. Na kuongeza kwamba limefanikiwa kuzikamata pikipiki 25 na vifaa vingine, pasipo kutoa taarifa zaidi. Mali imekuwa katika makabiliano na wimbi la wapiganaji wenye itikadi kali za Kiislamu lililozuka 2012, ambalo limegharimu maelfu ya maisha ya wanajeshi na raia tangu wakati huo. Pamoja na uwepo wa maelfu ya wanajeshi wa Ufaransa na vikosi vya Umoja wa Mataifa machafuko yameendelea na yameenea katika mataifa jirani ya Burkina Fasi na Niger.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Tanzania, Marekani zasaini makubaliano ya Dola Bilioni 3.14 kuimarisha sekta ya afya

Serikali za Tanzania na Serikali ya Marekani zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya ushirikiano katika sekta ya afya ya

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu