JPM aagiza kujengwa uzio kulizunguka eneo la Mererani.

In Kitaifa, Uchumi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameamuru eneo la Mererani Block A hadi D ujengwe ukuta wenye mlango mmoja na kamera zifungwe ili kuweza kukabiliana na wizi wa madini aina ya Tanzanite.

Ameyasema hayo hii leo Septemba 20, 2017 kwenye ziara ya kikazi mkoani Manyara katika Wilaya ya Simanjiro ambapo amesema ujenzi wa ukuta huo utasaidia kuondokna na wizi madini hayo hivyo serikali itaweza kukusanya mapato yake kikamilifu.

Rais Magufuli ametoa tamko la soko la Tanzanite kuwa litakua Simanjiro na si Arusha kama ilivyozoeleka na kusema wanunuzi watatakiwa kufunga safari kuelekea Simanjiro.

Na Rais Magufuli pia kabla ya kuzindua barabara mkoani Mannyara amewaomba wananchi hao kuitumia barabara hiyo ipasavyo bila kuiharibu kwani ni ya kila mmoja na kuwaomba wale wanaendesha vyombo vya moto kasi kutofanya hivo.

Rais Magufuli kwa upande mwingine ametoa hofu wakazi wa simanjiro kuhusiana na swala la maji wamuachie yeye kwani atahusika nalo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MABELE AHITIMISHA MAFUNZO YA JKT KWA VIJANA

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Rajabu Mabele, leo Septemba 18, 2026, amehitimisha rasmi mafunzo ya

Read More...

Safari ya Messi na Lamine Yamal Iliyotikisa Historia ya Soka

Soka lina uwezo wa kuandika simulizi ambazo hata waandishi wa riwaya hawawezi kuzibuni. Fainali ya Kombe la Dunia kati

Read More...

Serikali ya Marekani yaichangia Tanzania bilioni 2.63

Serikali ya Marekani imetoa zaidi ya Dola za Marekani milioni moja, sawa na takribani Sh. biliooni 2.63 ili kusaidia

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu