Nyalandu aomba kumsafirisha Tundu Lissu Marekani kwa Matibabu Zaidi.

In Afya, Kitaifa

Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu ameungana na viongozi wa Chadema kuweka kambi jijini Nairobi akisubiri ridhaa ya madaktari wa hospitali ya Nairobi kumpeleka Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu nchini Marekani kupata matibabu zaidi.

Nyalandu ambaye alifanikiwa kumuona Lissu na kuelezea hali yake, amesema kuwa madaktari wa hospitali ya Nairobi wamekuwa wazito kutoa ripoti maalum ya matibabu ya Lissu ili kumruhusu kumpeleka Marekani.

Mbunge huyo wa CCM ambaye amekuwa msitari wa mbele kushiriki kampeni ya kuchangisha fedha za kugharamia matibabu ya Lissu, ameonesha kuwa yeye ni mmoja kati ya watakaomsafirisha Lissu kwenda Marekani kupata huduma bora zaidi za matibau.

 “Tumekuwa #NairobiHospital tukisubiri MADAKTARI watoe RIPOTI ya mwenendo wa MATIBABU ya Mh #TunduLissu kwa minajili ya kuwapatia MADAKTARI BINGWA wa Marekani na kuona uwezekano wa Mh #TunduLissu kupatiwa RUFAA kwa matibabu zaidi NJE., LAKINI bado KALAMU zao ni nzito kuandika RIPOTI hii siku ya tatu tangu tuahidiwe. Binafsi, nimerudi NAIROBI tangu JANA kushiriki maandalizi ya uwezekano wa kumhamishia Mh #TunduLissu Marekani kwa ajili ya huduma yenye ubora zaidi, endapo MADAKTARI wa #NairobiHospital wangeridhia. Kesho asubuhi nitarejea hospitalini kusikiliza kauli ya mwisho ya MADAKTARI kuhusu RIPOTI hiyo.” Nyalandu ameandika Facebook

Lissu alijeruhiwa kwa risasi tano kati ya risasi zaidi ya thelathini alizoshambuliwa alipokuwa nyumbani kwake eneo la Area D mjini Dodoma, muda mfupi baada ya kutoka bungeni.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu