Rio Ferdinand kujiunga na ndondi baada ya kustaafu.

In Kimataifa, Michezo

Rio Ferdinand anazindua taaluma yake mpya kama mwanandondi miaka miwili baada ya kustaafu kutoka soka.

Hatua ya Rio mwenye umri miaka 38 kujiunga na ndondi imeiungwa mkono na kampuni ya kamari ya Betfair ambayo ilitangaza taraifa hizo leo Jumanne.

Mlinzi huyo wa zamani wa England na Manchester United pia ana kampuni yake ya nguo.

“Ninafanya hivi kwa sababu ni changamoto,” alisema Rio.” Nimeshinda mataji na sasa ninalenga kushinda mkanda.”

Amechapisha video kadha katika mitandao ya kijamii miezi ya hivi karibuni zinazomuanyesha akirusha ngumi na kupata mafunzo.

Aliyekuwa nahodha ya kikosi cha kriketi cha England Andrew Flintoff, pia naye alizindua taalumaa ya ndondi baada ya kustaafu, alipata ushindi mwaka 2012 dhidi ya Mmarekani Richard Dawson kwa pointi.

Ni kampuni ya Betfair iliyomuomba Ferdinand kuanzisha taaluma hiyo na itamsaidia kufuzu na kupata leseni ya bodi ya ndondi ya Uingereza kabla ya kuanza kujifunza na kushindana.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu