Rio Ferdinand kujiunga na ndondi baada ya kustaafu.

In Kimataifa, Michezo

Rio Ferdinand anazindua taaluma yake mpya kama mwanandondi miaka miwili baada ya kustaafu kutoka soka.

Hatua ya Rio mwenye umri miaka 38 kujiunga na ndondi imeiungwa mkono na kampuni ya kamari ya Betfair ambayo ilitangaza taraifa hizo leo Jumanne.

Mlinzi huyo wa zamani wa England na Manchester United pia ana kampuni yake ya nguo.

“Ninafanya hivi kwa sababu ni changamoto,” alisema Rio.” Nimeshinda mataji na sasa ninalenga kushinda mkanda.”

Amechapisha video kadha katika mitandao ya kijamii miezi ya hivi karibuni zinazomuanyesha akirusha ngumi na kupata mafunzo.

Aliyekuwa nahodha ya kikosi cha kriketi cha England Andrew Flintoff, pia naye alizindua taalumaa ya ndondi baada ya kustaafu, alipata ushindi mwaka 2012 dhidi ya Mmarekani Richard Dawson kwa pointi.

Ni kampuni ya Betfair iliyomuomba Ferdinand kuanzisha taaluma hiyo na itamsaidia kufuzu na kupata leseni ya bodi ya ndondi ya Uingereza kabla ya kuanza kujifunza na kushindana.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu