kiongozi wa upinzani senegal afunguliwa mshtaka, chama chake chafutwa

In Kimataifa

Waziri wa mambo ya ndani atangaza chama cha Sonko Pastef Les Patriotes kimefutwa

Raia wa Senegal waliachwa na mshangao siku ya Jumanne, siku moja baada ya kiongozi mkuu wa upinzani Ousmane Sonko kufunguliwa mashtaka mapya na chama chake kuvunjwa na kuharibu mipango yake ya kugombea urais.

Mwanasiasa mwenye umaarufu na mkosoaji mkuu wa Rais Macky Sall, ambaye ni maarufu sana miongoni mwa vijana amekabiliwa na msururu wa matatizo ya kisheria anayodai yanalenga kumweka nje ya siasa.

Nimekasirishwa nilitoka jana na kwenda kuandamana lakini kulikuwa hakuna mtu yeyote nje, alisema Thierno Mbaye, mfuasi wa Sonko aliyehojiwa na AFP katika mji mkuu wa Dakar. Sina matumaini tena aliongeza.

Siku ya Jumatatu Sonko alishtakiwa kwa kuchochea uasi, kudhoofisha usalama wa serikali, ushirikiano wa uhalifu na kundi la kigaidi na uhalifu mwingine.

Chini ya saa mbili baadaye waziri wa mambo ya ndani alitangaza chama chake cha PASTEF kingevunjwa.

Vyama vya siasa ni nadra kufutwa nchini Senegal. Mara ya mwisho ilifanyika mwaka 1966 kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKAGUA BARABARA YA SOMANGA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa asubuhi ya leo  Aprili 16, 2025 amewasili eneo la Somanga kukagua Miundombinu ya barabara kuu

Read More...

HATUTAWAACHIA CCM NAFASI TUTASHIRIKI UCHAGUZI MKUU – ACT WAZALENDO

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu amesema chama hicho kitashiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka

Read More...

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Gissima Nyamohanga Afariki Dunia 

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Gissima Nyamohanga amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika ajali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu