Mbaroni kwa kumua Mpenzi wake

In Kitaifa

JESHI la Polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam linamshikilia Musuguri Sylvester (29), mkazi wa Sinza, kwa tuhuma za mauaji ya aliyekuwa mpenzi wake, kisa wivu wa mapenzi.

Hayo yalisemwa jijini hapa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu, Kamishna wa Polisi, Simon Sirro wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Kamanda Sirro alisema tukio hilo lilitokea Machi 31, mwaka huu saa saa nne usiku katika maeneo ya Sinza Shekilango jijini Dar es Salaam.

Alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa baada ya ufuatiliaji wa taarifa ya tukio la mauaji ya mwanamke aliyejulikana kwa jina la Samira Masoud (34) aliyeuawa kwa kuchinjwa Machi 7, huko Kibamba na kisha mwili wake kuwekwa katika jaba la maji huku ukiwa umeharibika vibaya.

Aliongeza kuwa mtuhumiwa huyo katika mahojiano, amekiri kufanya mauaji ya mwanamke huyo na kusema sababu kubwa ilikuwa ni wivu wa kimapenzi baada ya kumfumania mpenzi wake akiwa chumbani na mwanamume mwingine ambaye hata hivyo mwanamume huyo alitoroka.

Alisema awali mtuhumiwa huyo aliwatumia ndugu wa marehemu ujumbe mfupi wa maandishi kwa kutumia namba ya simu ya marehemu ukisema: “Nendeni mkachukue maiti ya ndugu yenu itaozea ndani.”

“Mtaweza kuona ni ukatili wa namna gani uliofanywa na kijana huyu, hata kama mtu umemshika ugoni hupaswi kufanya tukio kama hili la kinyama,” alisema Kamanda Sirro na kuongeza kuwa upelelezi wa tukio hilo unaendelea na utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kwa hatua zaidi.

Chanzo:Habari Leo

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu