Mbaroni kwa kumua Mpenzi wake

In Kitaifa

JESHI la Polisi Kanda Maalumu Dar es Salaam linamshikilia Musuguri Sylvester (29), mkazi wa Sinza, kwa tuhuma za mauaji ya aliyekuwa mpenzi wake, kisa wivu wa mapenzi.

Hayo yalisemwa jijini hapa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu, Kamishna wa Polisi, Simon Sirro wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Kamanda Sirro alisema tukio hilo lilitokea Machi 31, mwaka huu saa saa nne usiku katika maeneo ya Sinza Shekilango jijini Dar es Salaam.

Alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa baada ya ufuatiliaji wa taarifa ya tukio la mauaji ya mwanamke aliyejulikana kwa jina la Samira Masoud (34) aliyeuawa kwa kuchinjwa Machi 7, huko Kibamba na kisha mwili wake kuwekwa katika jaba la maji huku ukiwa umeharibika vibaya.

Aliongeza kuwa mtuhumiwa huyo katika mahojiano, amekiri kufanya mauaji ya mwanamke huyo na kusema sababu kubwa ilikuwa ni wivu wa kimapenzi baada ya kumfumania mpenzi wake akiwa chumbani na mwanamume mwingine ambaye hata hivyo mwanamume huyo alitoroka.

Alisema awali mtuhumiwa huyo aliwatumia ndugu wa marehemu ujumbe mfupi wa maandishi kwa kutumia namba ya simu ya marehemu ukisema: “Nendeni mkachukue maiti ya ndugu yenu itaozea ndani.”

“Mtaweza kuona ni ukatili wa namna gani uliofanywa na kijana huyu, hata kama mtu umemshika ugoni hupaswi kufanya tukio kama hili la kinyama,” alisema Kamanda Sirro na kuongeza kuwa upelelezi wa tukio hilo unaendelea na utakapokamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kwa hatua zaidi.

Chanzo:Habari Leo

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu