Mvua zinazoendelea kunyesha zaleta Balaa

In Kimataifa

Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbali mbali Duniani zimeleta Madhara makubwa katika mji wa Edgecumbe uliopo kaskazini mwa nchi ya New Zealand.

Maelfu ya wakazi wameyakimbia makazi yao baada ya mafuriko makubwa yaliyozunguka mji huo kutokana na mvua kubwa iliyosababishwa na kimbunga cha Debbie kuyafunika makazi yao.

Kimbuka hicho pia kiliiathiri nchi ya Australia Alhamisi ya wiki iliyopita na kusababisha mito mbalimbali katika nchi hiyo kujaa kingo zake.

Katika mji wa Edgecumbe maji yanasemekana kufika hadi mita 2 katika baadhi ya maeneo. Hata hivyo hakuna ripoti yoyote ya kifo katika mafuriko hayo lakini kuna mtu mmoja ambaye alikuwa katika mto ndio anatafutwa na mpaka sasa hajaonekana.

Polisi katika mji huo wamesema watapiga doria katika maeneo yaliyohamwa na kuweka vizuizi kuwazuia raia wasije wakarudi. Tazama picha za mafuriko katika mji huo hapa chini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu