Mvua zinazoendelea kunyesha zaleta Balaa

In Kimataifa

Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbali mbali Duniani zimeleta Madhara makubwa katika mji wa Edgecumbe uliopo kaskazini mwa nchi ya New Zealand.

Maelfu ya wakazi wameyakimbia makazi yao baada ya mafuriko makubwa yaliyozunguka mji huo kutokana na mvua kubwa iliyosababishwa na kimbunga cha Debbie kuyafunika makazi yao.

Kimbuka hicho pia kiliiathiri nchi ya Australia Alhamisi ya wiki iliyopita na kusababisha mito mbalimbali katika nchi hiyo kujaa kingo zake.

Katika mji wa Edgecumbe maji yanasemekana kufika hadi mita 2 katika baadhi ya maeneo. Hata hivyo hakuna ripoti yoyote ya kifo katika mafuriko hayo lakini kuna mtu mmoja ambaye alikuwa katika mto ndio anatafutwa na mpaka sasa hajaonekana.

Polisi katika mji huo wamesema watapiga doria katika maeneo yaliyohamwa na kuweka vizuizi kuwazuia raia wasije wakarudi. Tazama picha za mafuriko katika mji huo hapa chini.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu