Rais John Magufuli leo anatarajiwa kupokea ripoti ya Kamati ya Pili ya wachumi na wanasheria, iliyochunguza madini yaliyopo kwenye makontena yenye mchanga wa madini.

In Kitaifa

Rais John Magufuli leo anatarajiwa kupokea ripoti ya Kamati ya Pili ya wachumi na wanasheria, iliyochunguza madini yaliyopo kwenye makontena yenye mchanga wa madini.

Anapokea ripoti hiyo ikiwa ni takribani siku 19 tangu alipokabidhiwa ripoti ya mchanga wa madini, iliyoibua madudu na hata kumlazimu kutengua uteuzi wa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, Kwa mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa kwa vyombo vya habari, Rais Magufuli atakabidhiwa ripoti hiyo leo asubuhi Ikulu, Dar es Salaam.

Kamati hiyo ilichunguza aina na viwango vya madini, yaliyomo kwenye mchanga wa madini uliomo ndani ya makontena, yaliyokuwa yamezuiliwa bandarini na Serikali yasisafirishwe kwenda nje ya nchi.

Baada ya kupokea, ripoti hiyo ilionesha mchanga uliokuwa unachunguzwa, ulikuwa na wastani wa kiasi cha thamani kati ya Sh bilioni 829.4 kwa kutumia viwango vya wastani wa chini na Sh trilioni 1.439 kwa kutumia viwango vya juu.

Kutokana na taarifa hiyo, Rais Magufuli aliivunja Bodi ya Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA), na kumsimamisha kazi Mtendaji Mkuu wa Wakala hiyo kutokana na kutosimamia ipasavyo, mchakato mzima wa usafirishaji mchanga wenye madini nje ya nchi na hivyo kuisababishia nchi hasara kubwa.

Aidha, mbali na kutengua uteuzi wa Waziri Muhongo, alivunja Bodi ya TMAA na kumsimamisha kazi Mtendaji Mkuu wake. Rais Magufuli pia aliviagiza vyombo vya dola, kuwachunguza na kuwachukulia hatua watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini na wengine waliohusika na kushindwa kusimamia vema mchakato mzima wa usafirishaji wa mchanga wenye madini nje ya nchi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKAGUA BARABARA YA SOMANGA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa asubuhi ya leo  Aprili 16, 2025 amewasili eneo la Somanga kukagua Miundombinu ya barabara kuu

Read More...

HATUTAWAACHIA CCM NAFASI TUTASHIRIKI UCHAGUZI MKUU – ACT WAZALENDO

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu amesema chama hicho kitashiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka

Read More...

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Gissima Nyamohanga Afariki Dunia 

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Gissima Nyamohanga amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika ajali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu