Rais wa Venezuela aongeza marufuku ya kutotoka nje kwa siku zengine 30.

In Kimataifa

Rais wa Venezuela Nicolas Maduro ametangaza kuongeza kwa siku thelathini hatua za vizuizi vya kutoka nje kutokana na janga la virusi vya corona.

Maduro aliweka vizuizi vya kwanza mnamo Machi 13 na awali aliwahi kuongeza vizuizi hivyo hadi katikati ya mwezi Aprili.

Rais huyo wa kisosholisti amesema visa 423 vimeripotiwa huku watu kumi wakiaga dunia.

Ila idadi hiyo imetiliwa shaka na mpinzani wake Juan Guaido anayesema idadi ya walioambukizwa na kufariki iko juu mno kuliko ilivyotangazwa kutokana na kuanguka kwa mfumo wa afya nchini humo kutokana na miaka ya mzozo wa kiuchumi.

Masharti ya vikwazo hivyo ni kwamba mtu anaweza kutoka nje tu iwapo anakwenda hospitali au kununua chakula.

Venezuela pia imetangaza kurefusha hadi Juni 12 ndege kuingia na kutoka nchini humo

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu