Rais wa Venezuela aongeza marufuku ya kutotoka nje kwa siku zengine 30.

In Kimataifa

Rais wa Venezuela Nicolas Maduro ametangaza kuongeza kwa siku thelathini hatua za vizuizi vya kutoka nje kutokana na janga la virusi vya corona.

Maduro aliweka vizuizi vya kwanza mnamo Machi 13 na awali aliwahi kuongeza vizuizi hivyo hadi katikati ya mwezi Aprili.

Rais huyo wa kisosholisti amesema visa 423 vimeripotiwa huku watu kumi wakiaga dunia.

Ila idadi hiyo imetiliwa shaka na mpinzani wake Juan Guaido anayesema idadi ya walioambukizwa na kufariki iko juu mno kuliko ilivyotangazwa kutokana na kuanguka kwa mfumo wa afya nchini humo kutokana na miaka ya mzozo wa kiuchumi.

Masharti ya vikwazo hivyo ni kwamba mtu anaweza kutoka nje tu iwapo anakwenda hospitali au kununua chakula.

Venezuela pia imetangaza kurefusha hadi Juni 12 ndege kuingia na kutoka nchini humo

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu