Waziri wa Madini Dkt Doto Biteko, amesema kuwa kuna
matukia kadhaa ya watu wanaochejua Dhahabu kuvamiwa na
kuibiwa na kuwahakikishia wachimbaji hao kuwa serikali
inalaani vikali na kutoa onyo kuwa atakayejaribu kuvamia na
kumuibia mchimbaji yeyote atakamatwa na kuchukuliwa hatua
kali.
Aidha Waziri Biteko amesema kamati ya Ukaguzi wa Madini ya
Jumuiya ya Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR) ina jukumu
kubwa la kuhakikisha kuwa, madini yanayochimbwa katika nchi
wanachama wa jumuiya hiyo yanakuwa chachu ya amani na si
migogoro.
Dkt.Biteko ametoa rai hiyo wakati akifungua Mkutano wa 20 wa
Kamati ya Ukaguzi wa Madini ya Jumuiya ya Ukanda wa
Maziwa Makuu (ICGLR) ambapo Tanzania ni mwenyeji wa
mkutano huo unaofanyika mjini Bukoba Mkoa wa Kagera.



