Serikali imesema kuwa gharama za matibabu ya kusafisha figo
ni kubwa kiasi kwamba hazibebeki,hivyo inafanya mapitio ya
kuzipunguza.
Ahadi hiyo imetolewa bungeni leo Juni 21 na Naibu Waziri wa
Afya Dk Godwin Mollel,akisema kuwa kwa sasa gharama hizo
zinafikia Shilingi laki tisa,kiasi ambacho ni kikubwa kwa watu
wa kipato cha chini.
Ametoa kauli hiyo wakati akijbu swali la nyongeza la Mbunge
wa Viti Maalumu Mariam Kisangi,ambaye ameomba gharama
hizo zipunguzwe,huku kwa wagonjwa wanaotumia bima ya afya
wapate vifurushi vya matibabu hayo.