Mkurugenzi mkuu wa shirika la Reli Tanzania TRC Masanja
Kadogosa amesema kuwa mwisho wa Mwezi April Treni ya
umeme ya majaribio itaanza kutembea kutoka Dar es salaam
hadi mkoani Morogoro ikiwa ni kwa ara ya kwanza kwa kipande
hicho.
Ameyasema hayo mbele ya Waziri wa Ujenzi na uchukuzi Prof
Makame Mbarawa,wakati wa zoezi uwekaji wa jiwe la msingi la
ujenzi wa Reli ya kisasa kutoka Makutupora mkoani Dodoma
hadi Tabora.
Kwa upande wake waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor
Mbarawa,amemtaka mkandarasi kukamilisha mradi huo kwa
wakati,na hatavumilia kuona uzembe kwani serikali imeshalipa
fedha zote za maradi huo.