Undani wa Taarifa za Msanii wa Nigeria D’Banj kutembea na Mpenzi wa Msanii wa Marekani T.I

In Burudani

EEEEH bhana kama una kumbukumbu nzuri nishakupa taarifa za T.I kuachana na mkewe Tiny ambaye wamekuwa pamoja kwenye ndoa miaka 6 na kuachana December mwaka jana 2016.

Rapper T.I

Sasa baada ya T.I kuachana na mama toto wake alihamishia penzi lake kwa Video Queen maarufu ajulikanaye kama Bernice Burgos ambaye alihusika kama model kwenye Video ya DjKaled Do you mind ambayo amemshirikisha Chris Brown, Nicki Minaj, August Alsina, Jeremih Future na  Rick Ross

Sasa kuna taarifa kwamba Msanii wa Nigeria  Oladapo Daniel Oyebanjo maarufu kama D’banj naye anakula Mrembo huyo.

Bernice Burgos

Taarifa hizo zimeongezwa na nguvu na Uwepo wa DBanj na Mrembo huyo kwenye bata la pamoja huko katika  visiwa vya Bahamas kaskazini mwa Kuba

D’BANJ

Kupitia mtandao wa Snapchat model huyo  alitupia picha akiwa ameshikwa kiuno na D’banj.

Ila pamoja na minong’ono hiyo kwamba wanakwich DBanj na Model huyo kwa upande wa DBanj yeye anasema wanafanya Video ya wimbo wake mpya uitwao  ‘Be With You’ ambao Bernice ametumika kama model.

DBanj anayemiliki DB Records amesema ataendelea kufanya kazi na watu wenye viwango vya Kimataifa kwa ajili ya kuhakikisha Kazi zake zinafika anapotaka.

MREMBO HUYO ALIKULA SHAVU KWENYE VIDEO HII HAPA CHINI

BAADHI YA PICHA ZA MREMBO HUYO

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKAGUA BARABARA YA SOMANGA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa asubuhi ya leo  Aprili 16, 2025 amewasili eneo la Somanga kukagua Miundombinu ya barabara kuu

Read More...

HATUTAWAACHIA CCM NAFASI TUTASHIRIKI UCHAGUZI MKUU – ACT WAZALENDO

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu amesema chama hicho kitashiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka

Read More...

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Gissima Nyamohanga Afariki Dunia 

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Gissima Nyamohanga amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika ajali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu