Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa walioshikiliwa mateka waachiwa.

In Kimataifa

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imearifu kuwa wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa waliokuwa wakishikiliwa mateka na wakimbizi kutoka Sudan Kusini, wameachiwa huru wakiwa salama.
Wafanyakazi hao 16 walikuwa wakishikiliwa na kundi la waasi wa zamani kutoka Sudan Kusini, waliokuwa wafuasi wa makamu wa rais wa zamani wa nchi hiyo Riek Machar, na ambao waliikimbia nchi yao baada ya kuzuka mapigano baina yao ya wanajeshi wa serikali ya Rais Salva Kiir.
Wakimbizi hao walikuwa wakishinikiza kupelekwa katika nchi nyingine, kuepuka msongamano katika kambi ndogo wanakohifadhiwa Mashariki mwa Kongo.
Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa Wasudan Kusini wapatao milioni tatu wameyapa kisogo maskani yao, wakikimbia vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyoripuka mwaka 2013, baada ya Rais Kiir kumfukuza makamu wake, Riek Machar.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu