Wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa walioshikiliwa mateka waachiwa.

In Kimataifa

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imearifu kuwa wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa waliokuwa wakishikiliwa mateka na wakimbizi kutoka Sudan Kusini, wameachiwa huru wakiwa salama.
Wafanyakazi hao 16 walikuwa wakishikiliwa na kundi la waasi wa zamani kutoka Sudan Kusini, waliokuwa wafuasi wa makamu wa rais wa zamani wa nchi hiyo Riek Machar, na ambao waliikimbia nchi yao baada ya kuzuka mapigano baina yao ya wanajeshi wa serikali ya Rais Salva Kiir.
Wakimbizi hao walikuwa wakishinikiza kupelekwa katika nchi nyingine, kuepuka msongamano katika kambi ndogo wanakohifadhiwa Mashariki mwa Kongo.
Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa Wasudan Kusini wapatao milioni tatu wameyapa kisogo maskani yao, wakikimbia vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyoripuka mwaka 2013, baada ya Rais Kiir kumfukuza makamu wake, Riek Machar.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKAGUA BARABARA YA SOMANGA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa asubuhi ya leo  Aprili 16, 2025 amewasili eneo la Somanga kukagua Miundombinu ya barabara kuu

Read More...

HATUTAWAACHIA CCM NAFASI TUTASHIRIKI UCHAGUZI MKUU – ACT WAZALENDO

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu amesema chama hicho kitashiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka

Read More...

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Gissima Nyamohanga Afariki Dunia 

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Gissima Nyamohanga amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika ajali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu