Wanamgambo 15 Wa Al Shabaab Wauawa na Wakenya

In Kimataifa

KENYA: Wanajeshi wa KDF wamewauwa wanamgambo 15 wa Al shabaab usiku wa kuamakia jana wakati walipovamia kambi yao ya Katamaa umbali wa kilomita 100 kutoka mpaka wa Kenya na Somalia katika mji wa Elwark.

Akiongea na waandishi wa Habari, msemaji wa jeshi la KDF kanali Joseph Owuoth ameelezea kuwa wanajeshi  walifanikiwa kuvamia  na kuharibu kambi iliyokuwa na magaidi hao kwa kutumia mizinga waliyo kuwa nayo.

Aidha joseph amewahakikishia wakenya kuwa  serikali itaendelea kushirikiana na jeshi la Somalia ili  kupambana na magaidi huku akisema tayari hali ya kawaida imerudi katika miji kaadha nchini Somalia ikiwemo mji wa kismayu.

Inaaminika kuwa baadhi ya wanamgambo walifanikiwa kutoroka wakiwa na majeraha huku wanajeshi wa KDF wakiwa wapo salama na hakuna anaye uguza jeraha lolote.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu