Watu 9 Wahofiwa kufa maji huko Zanzibar

In Kitaifa

WATU tisa hawajulikani waliko huku 44 wameokolewa baada ya mashua yao ya uvuvi kuzama pwani mwa kisiwa cha Zanzibar.

Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Upelelezi  amesema harakati za uokoaji bado zinaendelea.

“Tunafahamu, kuwa ajali hiyo ilisababishwa na upepo na mawimbi makali yaliyosababisha mashua hiyo kuzama,” alisema.

Manusura mmoja aliwaambia waokoaji kuwa takriban watu 53 waliondoka kwenda kuvua samaki jana jioni wakati bahari ilikuwa tulivu lakini hali ya hewa ilibadilika na kusababisha mawimbi makali na kwamba hajawaona wenzake tangu ajali hiyo itokee.

Uvuvi ni shughuli kubwa ya kiuchumi kisiwani Zanzibar lakini mashua nyingi zimechakaa na hivyo husababisha ajali nyingi kila mara.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu