Watu 9 Wahofiwa kufa maji huko Zanzibar

In Kitaifa

WATU tisa hawajulikani waliko huku 44 wameokolewa baada ya mashua yao ya uvuvi kuzama pwani mwa kisiwa cha Zanzibar.

Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Upelelezi  amesema harakati za uokoaji bado zinaendelea.

“Tunafahamu, kuwa ajali hiyo ilisababishwa na upepo na mawimbi makali yaliyosababisha mashua hiyo kuzama,” alisema.

Manusura mmoja aliwaambia waokoaji kuwa takriban watu 53 waliondoka kwenda kuvua samaki jana jioni wakati bahari ilikuwa tulivu lakini hali ya hewa ilibadilika na kusababisha mawimbi makali na kwamba hajawaona wenzake tangu ajali hiyo itokee.

Uvuvi ni shughuli kubwa ya kiuchumi kisiwani Zanzibar lakini mashua nyingi zimechakaa na hivyo husababisha ajali nyingi kila mara.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu