Waziri wa Ulinzi wa Ukraine Kung’atuliwa

In Kimataifa

Mbunge mwenye ushawishi mkubwa nchini Ukraine amesema waziri wa ulinzi wa nchi hiyo Oleksii Reznikov ataondolewa na nafasi yake kuchukuliwa na mkuu wa ujasusi jeshini, kutokana na tuhuma za ufisadi jeshini.

Waziri huyo wa ulinzi wa Ukraine amekuwa akikabiliwa na shinikizo la kumtaka ajiuzulu, baada ya kuibuka tuhuma za ufisadi jeshini, lakini amekuwa akikaidi shinikizo hilo, akisema ataachia ngazi ikiwa tu atatakiwa kufanya hivyo na Rais Volodymyr Zelenskiy.

Hata hivyo, mbunge mmoja mwenye nguvu nchini Ukraine, David Arakhamia amesema jana jioni kuwa Reznikov angeondolewa kutokana na kashfa hiyo ya ufisadi ambayo imemlazimisha naibu wake kujiuzulu.

Arakhamia amesema vita vinaweka ushawishi katika sera zinazohusu wafanyakazi, na kwamba mkuu wa ujasusi jeshini Kyrilo Budanov angeteuliwa kuwa waziri mpya wa ulinzi. Mbunge huyo amesema waziri Reznikov atahamishiwa katika wizara nyingine, bila hata hivyo kubainisha muda yatakapofanyika mabadiliko hayo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu