Waziri wa Ulinzi wa Ukraine Kung’atuliwa

In Kimataifa

Mbunge mwenye ushawishi mkubwa nchini Ukraine amesema waziri wa ulinzi wa nchi hiyo Oleksii Reznikov ataondolewa na nafasi yake kuchukuliwa na mkuu wa ujasusi jeshini, kutokana na tuhuma za ufisadi jeshini.

Waziri huyo wa ulinzi wa Ukraine amekuwa akikabiliwa na shinikizo la kumtaka ajiuzulu, baada ya kuibuka tuhuma za ufisadi jeshini, lakini amekuwa akikaidi shinikizo hilo, akisema ataachia ngazi ikiwa tu atatakiwa kufanya hivyo na Rais Volodymyr Zelenskiy.

Hata hivyo, mbunge mmoja mwenye nguvu nchini Ukraine, David Arakhamia amesema jana jioni kuwa Reznikov angeondolewa kutokana na kashfa hiyo ya ufisadi ambayo imemlazimisha naibu wake kujiuzulu.

Arakhamia amesema vita vinaweka ushawishi katika sera zinazohusu wafanyakazi, na kwamba mkuu wa ujasusi jeshini Kyrilo Budanov angeteuliwa kuwa waziri mpya wa ulinzi. Mbunge huyo amesema waziri Reznikov atahamishiwa katika wizara nyingine, bila hata hivyo kubainisha muda yatakapofanyika mabadiliko hayo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKAGUA BARABARA YA SOMANGA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa asubuhi ya leo  Aprili 16, 2025 amewasili eneo la Somanga kukagua Miundombinu ya barabara kuu

Read More...

HATUTAWAACHIA CCM NAFASI TUTASHIRIKI UCHAGUZI MKUU – ACT WAZALENDO

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu amesema chama hicho kitashiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka

Read More...

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Gissima Nyamohanga Afariki Dunia 

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Gissima Nyamohanga amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika ajali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu