Wenger awatupia lawama waamuzi Uingereza.

In Kimataifa, Michezo

Kocha wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger ametoa lawama kwa waamuzi kwa kusema viwango vya usimamizi wa mechi katika ligi kuu ya Uingereza vimeendelea kudorora mwaka baada ya mwaka.

Lawama za Wenger zinakuja baada kipigo cha mabao 3-1 ambacho Arsenal walipata jana kutoka kwa Manchester City katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa kwenye uwanja wa Etihad.

Wenger anaamini mshambuliaji wa Man City Raheem Sterling alijiangusha na kupewa penati iliyopigwa na Sergio Aguero dakika ya 50 ambayo iliwasaidia wenyeji kupata bao la pili.

”Nafikiri waamuzi hawafanyi kazi ya kutosha amesema, viwango vinashuka kila msimu kwa sasa na kwa jumla haikubaliki,” alisema Wenger.

City walipata bao la tatu lililofungwa na Gabriel Jesus dakika ya 74 lakini Wenger anaamini bao hilo halikufaa kukubaliwa kwani lilikuwa la kuotea.

Matokeo hayo yameifanya Manchester City kuzidi kujikita kileleni mwa EPL wakiwa na pointi 11 huku Arsenal wakiwa na katika nafasi ya 6 wakiwa na pointi 19 baada ya kucheza michezo 11.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu