Ziara ya Justin Bieber “PURPOSE WORLD TOUR” iliyofanyika mwaka jana na mwaka huu imeingiza dola milioni 200 ambazo ni sawa na Fedha za Kitanzania zaidi ya 440,000,000,000.
Ziara hiyo ilianza March 2016. Hadi sasa zaidi ya tiketi milioni 2.2 zimeuzwa kwaajili ya show katika maeneo 122 duniani.
Ziara hiyo ilianza March 9, 2016 huko Seattle na awamu ya kwanza ilimalizika Nov. 29. Ziara hiyo ilianza tena Feb. 15, 2017 huko Monterrey, Mexico.
Hadi mwishoni mwa 2016, Bieber alikamata nafasi ya 5 ya orodha ya Billboard ya ziara 25 zilizoingia fedha nyingi zaidi.
