Fenerbahce wanamtaka mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa.

In Kimataifa, Michezo

Klabu ya Fenerbahce ya Uturuki imefanya mazungumzo na wawakilishi wa mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa kuhusu uwezekano wa kumchukua kwa mkopo.

Costa, 28, amesalia nchini Brazil na amekataa kurejea England.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania alishindwa kuhama kutoka kwa mabingwa hao wa Ligi ya Premia kabla ya siku ya mwisho ya kuhama wachezaji katika ligi nyingi kuu Ulaya.

Hata hivyo, dirisha la uhamisho wa wachezaji Uturuki bado liko wazi na litafungwa baadaye leo Ijumaa.

Duru zinasema baada ya mazungumzo ya kwanza kufanyika, uwezekano wake kuhama ni finyu, lakini mazungumzo bado yanaendelea.

Costa ameambia na meneja wa Chelsea Antonio Conte ajitafutie klabu itakayomchukua.

Alitaka kurejea Atletico Madrid majira ya joto lakini klabu hiyo ya Uhispania hairuhusiwi kuwasajili wachezaji kutokana na marufuku waliyowekewa hadi Januari.

Hii ina maana kwamba Costa anaweza tu kuhamia klabu hiyo Januari mwakani.

Mshambuliaji huyo hajajumuishwa kwenye orodha ya wachezaji wa Chelsea watakaoshiriki Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu