Deontay Wilder: Anthony Joshua haniwezi.

In Kimataifa, Michezo

Bingwa wa ndondi katika uzani wa WBC Deontay Wilder anasema kuwa atampiga Anthony Joshua nyumbani kwake Uingereza.

Wilder mwenye umri wa miaka 32 alitetea taji lake dhidi ya Bermaine Stiverne siku ya Jumamosi , wiki moja baada ya Joshua kuhifadhi taji lake la ukanda wa WBA na IBF dhidi ya Carlos Takam mjini Cardiff.

”Viwanja vilivyojaa watu vinaonekana vizuri lakini Mecca ya ndondi ipo Marekani”, Wilder aliambia BBC Sport.

”Lakini kama unataka kusalia nyumbani kama msichana mdogo mfalme huyu hajali kuja na kumwangusha bingwa”.Katika mahojiano na BBC Radio 5, Wilder alimshutumu promota Eddie Hearn kwa kuwadanganya mashabiki kwamba Joshua ndio bondia bora katika uzani mzito duniani.

”Iwapo Joshua ndio bora, na bingwa , Waingereza wanafaa kumwambia ajitokeze na apigane ndio mujue kwamba yeye ndio bora”.

”Moyo wangu unaniambia kwamba mimi ndio bora na kama sio bora basi ningependa aliye bora aje anionyeshe”

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu