Mapigano kati ya makundi pinzani ya Libya mashariki mwa Tripoli yameingia siku ya pili jana

In Kimataifa
Mapigano kati ya makundi pinzani ya Libya mashariki mwa Tripoli yameingia siku ya pili jana, na kuwazuia wakaazi kurejea majumbani kwao.
Mapigano yalizuka Jumapili wakati makundi yenye silaha yanayoipinga serikali inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa mjini Tripoli yalijaribu kuingia katika mji huo mkuu na wakakabiliwa na makundi hasimu ambayo yanaegemea upande wa serikali hiyo.
Wizara ya afya ya Libya imethibitisha kuwa karibu watu wanne wameuawa na wengine 21 wamejeruhiwa katika mapigano hayo.
 Serikali ya Umoja wa Kitaifa imeshindwa kuweka utulivu tangu ilipowasili mjini Tripoli Machi mwaka jana. Serikali hiyo inapingwa na makundi ambayo yanadhibiti mashariki mwa Libya, ambako kamanda wa kijeshi Khalifa Haftar amekuwa akiimarisha nafasi yake kwa kuwateua mameya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WAZIRI MKUU MAJALIWA AKAGUA BARABARA YA SOMANGA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa asubuhi ya leo  Aprili 16, 2025 amewasili eneo la Somanga kukagua Miundombinu ya barabara kuu

Read More...

HATUTAWAACHIA CCM NAFASI TUTASHIRIKI UCHAGUZI MKUU – ACT WAZALENDO

Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu amesema chama hicho kitashiriki kikamilifu katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka

Read More...

Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Gissima Nyamohanga Afariki Dunia 

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Mhandisi Gissima Nyamohanga amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika ajali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu