TRA Wawahurumia Serengeti Boys na Kuliachia basi la TFF Lenye Deni kubwa

In Michezo

Mamlaka ya mapato nchini, TRA imeliachia basi la shirikisho la soka nchini, TFF lililokuwa limekamatwa na wakala wake wa udalali, Yono kutokana na limbikizo la madeni. Kampuni ya Yono ililishikilia kwa muda basi hilo jana.

Taarifa ya TFF kupitia mitandao ya kijamii imesema: Nathibitisha kuwa Kampuni ya Udalali ya Yono ambayo ni Wakala wa TRA imetangaza kuliachia gari mara moja basi linalotumiwa na wachezaji wa Serengeti Boys na wameomba nilifuate hata sasa, usiku huu. Wamefuata amri ya TRA. Tutalifuata asubuhi, ili liendelee na shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwapeleka vijana wetu Airport kuwahi ndege kwani vijana wetu wanatarajia kuondoka jioni.

Naye Rais wa TFF, Jamal Malinzi ametweet: Basi la TFF limeachiwa usiku huu.Suala hili la kodi tukijaliwa tutalimaliza vizuri tu kwa majadiliano.Usikimbilie kuhukumu.”

Awali wao wenye TRA waliandika: TRA inasikitishwa na kitendo cha mmoja wa mawakala wa kudai madeni kwa kukamata gari ya Serengeti Boys bila kujali wala kuzingatia utaratibu. Imethibitisha agizo la kuachiwa kwa gari hiyo limetekelezwa, wakati taratibu zingine za kiutendaji zikiwa zinaendelea kwa wahusika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

NIFFER NA CHAVALA WAACHIWA HURU NA MAHAKAMA

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imewaachia huru leo mchana vijana Jennifer Jovin (26), maarufu kama

Read More...

Trump kukutana na viongozi wa Rwanda na DR Kongo Alhamisi

Rais wa Marekani Donald Trump atakutana na viongozi wa Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo siku ya Alhamisi

Read More...

SERIKALI YAAGIZWA KUFUTWA KWA LESENI 73.

Serikali kupitia Wizara ya Madini imeielekeza Tume ya Madini kufuta jumla ya leseni 73ambazo maeneo yake hayajaendelezwa. Hayo yameelezwa leo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu