Zitto na Mchinjita wafunguka kutekwa kwa Abdul Nondo.

In Kitaifa, Siasa

Jeshi la Polisi Tanzania limesema Mwenyekiti wa Ngome ya
Vijana wa chama cha ACT Wazalendo Ndugu Abdul Nondo
alietekwa Alfajiri ya Tar moja Dec,ametelekezwa maeneo ya
fukwe za Coco, Kindondoni jijini Dar es Salaam na watu ambao
hawafahamu.


Polisi wamesema baada ya kutelekezwa katika eneo hilo, Nondo
alisimamisha bodaboda na kumwelekeza amfikishe katika ofisi
za chama chake zilizopo Magomeni,Jijini Dar es Salaam
walifika muda wa saa tano usiku.


Kwa mujibu wa taarifa hiyo, baada ya kufika katika ofisi hizo,
Nondo alionana na viongozi wake na kupelekwa hospitali kwa
ajili ya uchunguzi wa afya yake.

Makamu mwenyekiti wa ACT Wazalendo Isihaka Mchinjita,ni
miongoni mwa waliofika katika hospitali ya Aghakani kumjulia
hali Nondo na amezugumza baadhi ya mambo.

Kwa upande wake Kiongozi mstaafu wa chama hicho ndugu
Zitto Kabwe akizungumzia tukio hilo,amewataka watanzania
kuendelea kumwombea Nondo hali yake iwe sawa,na atapopata
nafuu ataweza kuelezea mwenyewe kile kilichotokea.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

NIFFER NA CHAVALA WAACHIWA HURU NA MAHAKAMA

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imewaachia huru leo mchana vijana Jennifer Jovin (26), maarufu kama

Read More...

Trump kukutana na viongozi wa Rwanda na DR Kongo Alhamisi

Rais wa Marekani Donald Trump atakutana na viongozi wa Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo siku ya Alhamisi

Read More...

SERIKALI YAAGIZWA KUFUTWA KWA LESENI 73.

Serikali kupitia Wizara ya Madini imeielekeza Tume ya Madini kufuta jumla ya leseni 73ambazo maeneo yake hayajaendelezwa. Hayo yameelezwa leo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu