Waziri Mkuu wa DRC ajiuzulu kupisha uteuzi mwingine.

In Kimataifa

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Samy Badibanga ametangaza kujiuzulu.

Hatua hii imekuja baada ya rais Joseph Kabila siku ya Jumanne, kulihotubia bunge na kuahidi kumteua Waziri Mkuu mpya ndani ya saa 48.

Badibanga mwenye umri wa miaka 54 aliteuliwa katika nafasi hiyo mwezi Novemba mwaka 2016 baada ya jitihada za kuwepo kwa mazungumzo ya kisiasa chini ya mjumbe wa Umoja wa Afrika.

Baada ya kutiwa saini kwa mkataba wa kisiasa kati ya serikal na upinzani mwisho wa mwezi Desemba mwaka 2016 baada ya upatanishi, wa Maaskofu wa Kanisa Katoliki,ilikubaliwa kuwa Waziri Mkuu mpya ateuliwe kutoka upinzani.

Muda wa rais Kabila kukaa madarakani ulikamilika mwaka uliopita lakini kwa sababu ya mzozo wa kisiasa nchini humo, ameendelea kukaa madarakani baada ya Tume ya Uchaguzi kusema haina fedha za kuandaa Uchaguzi Mkuu.

Upinzani wamekuwa wakisema kuwa wanataka kupendekeza jina moja huku upande wa serikali ukisema kuwa upinzani kupendekeza majina matatu na rais kumteua mmoja.

Hata baada ya hotuba ya rais Kabila, wanasiasa wa upinzani wameonekana kutounga mkono na juhudi za rais Kabila kuwa Waziri Mkuu atapatikana baada ya  saa 48 na kupitisha uundwaji wa serikali ya mpito.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu