Waziri Mkuu wa DRC ajiuzulu kupisha uteuzi mwingine.

In Kimataifa

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Samy Badibanga ametangaza kujiuzulu.

Hatua hii imekuja baada ya rais Joseph Kabila siku ya Jumanne, kulihotubia bunge na kuahidi kumteua Waziri Mkuu mpya ndani ya saa 48.

Badibanga mwenye umri wa miaka 54 aliteuliwa katika nafasi hiyo mwezi Novemba mwaka 2016 baada ya jitihada za kuwepo kwa mazungumzo ya kisiasa chini ya mjumbe wa Umoja wa Afrika.

Baada ya kutiwa saini kwa mkataba wa kisiasa kati ya serikal na upinzani mwisho wa mwezi Desemba mwaka 2016 baada ya upatanishi, wa Maaskofu wa Kanisa Katoliki,ilikubaliwa kuwa Waziri Mkuu mpya ateuliwe kutoka upinzani.

Muda wa rais Kabila kukaa madarakani ulikamilika mwaka uliopita lakini kwa sababu ya mzozo wa kisiasa nchini humo, ameendelea kukaa madarakani baada ya Tume ya Uchaguzi kusema haina fedha za kuandaa Uchaguzi Mkuu.

Upinzani wamekuwa wakisema kuwa wanataka kupendekeza jina moja huku upande wa serikali ukisema kuwa upinzani kupendekeza majina matatu na rais kumteua mmoja.

Hata baada ya hotuba ya rais Kabila, wanasiasa wa upinzani wameonekana kutounga mkono na juhudi za rais Kabila kuwa Waziri Mkuu atapatikana baada ya  saa 48 na kupitisha uundwaji wa serikali ya mpito.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu